Habari

Kalonzo ndiye ataupeleka upinzani Bondo

Na CECIL ODONGO November 3rd, 2025 Kusoma ni dakika: 1

VIONGOZI wa upinzani watavamia Bondo kwa kishindo Alhamisi hii kumwomboleza na kumuenzi aliyekuwa waziri mkuu marehemu Raila Odinga.

Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka alitangaza kuwa watafika Kangó ka Jaramogi ambako Raila alizikwa na nyumbani kwake Opoda kumwomboleza.
Alizungumza kwenye hafla moja na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambaye bado haijafahamika iwapo atakuwa kwenye ziara hiyo.