Kimataifa

Urusi yaishambulia Ukraine na kuwaacha maelfu kwenye baridi kali

Na MASHIRIKA February 4th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KYIV, UKRAINE

MAELFU wameachwa bila makazi na kwenye gizani baada ya Urusi kuishambulia Ukraine kwa makombora yenye masafa marefu.

Makombora hayo pamoja na ndege zisizo na rubani zilishambulia kituo cha nishati mjini Kyiv pamoja na maeneo mengine.

“Hili ni pigo kubwa sana kwetu mwaka huu,” kampuni ya nishati ya kibinafsi ya DTEK ilisema.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema Urusi imeamua kufufua vita hivyo badala ya kutumia njia ya kidiplomasia kuvimaliza.

Haya yanajiri wiki chache baada ya Rais wa Urusi Vladimir Putin kukubaliana na mwenzake wa Amerika Donald Trump kwamba itaacha kushambulia miundo mbinu ya nishati Ukraine msimu huu wa baridi.