Raha Gen Z wakishinda uchaguzi Bangladesh
VIJANA wa Gen Z Bangladesh wanaendelea kusherehekea baada ya kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo mnamo Alhamisi Februari 12, 2026.
Ushindi huo unatarajiwa kuleta udhabiti katika nchi hiyo ambayo ilikuwa imeathiriwa na wimbi la maandamano la kupigania uongozi bora mnamo 2024.
Uchaguzi wa ubunge uliofanyika Alhamisi ulikuwa wa kwanza kuandaliwa tangu Gen Z washiriki maandamano 2024 yaliyomwondoa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu Sheikh Hasina.
Maandamano hayo ambayo yalisababisha vifo vya vijana wengi yalivuruga uchumi wa taifa hilo na kusababisha viwanda viporomoke.
Vijana wengi waliuawa na maafisa wa usalama wakati wa maandamano hayo.
Huu ulikuwa uchaguzi wa kwanza uliokuwa ukiandaliwa na taifa baada ya maandamano ya Gen Z kuyatikisa mataifa mbalimbali.
Nepal ambayo pia iliathirika, itakuwa ikiandaa uchaguzi wake mwezi ujao.
Kwenye uchaguzi wa ubunge chama cha BNP ambacho ni cha Gen Z kilitwaa viti 209 kati ya 300 na kupata ushindi wa zaidi ya theluthi mbili.
“Licha ya kushinda ubunge kwa kura nyingi, hakuna hafla ambayo itaandaliwa ya umma ya sherehe. Wafuasi wetu wanaombwa waende makanisani, misikitini, hekaluni na maeneo mengi ya kuabudu,” ikasema taarifa ya chama hicho.
BNP kinaongozwa na Tarique Rahman, 60 mwanawe Waziri Mkuu wa zamani Khaleda Zia na rais wa zamani Ziaur Rahman.
Tarique ambaye sasa atakuwa waziri mkuu amekuwa akikita kampeni zake katika kuimarisha mapato ya raia maskini, kubadilisha katiba ili yule atakayeshikilia wadhifa wa waziri mkuu awe anahudumu miaka 10 pekee, kuimarisha uchumi kupitia ushirikiano na wawekezaji na kukumbatia sera kali za kupambana na ufisadi.
Shafiqur Rahman, mkuu wa chama cha Islamist Jamaat-e-Islami, alikiri kuwa wameshindwa baada ya kujizolea viti 68. Rahman alisema kama upinzani watatekeleza majukumu yao ipasavyo badala tu ya kuyafumbia macho maovu ya raia.
Chama cha NCP ambacho kilikuwa kikiongozwa na wanaharakati vijana ambao walitekeleza majukumu muhimu katika kumwondoa Hasina, nacho kilipata viti vitano na kiliwania viti 30.
Kilisena kitatekeleza majukumu yake ipasavyo mradi tu ya kuyafumbia macho maovu ya raia.
Chama cha Awami League, kilichokuwa kikiongozwa na Hasina na kimekuwa uongozini kwa miaka 15, kilizuiwa kushiriki kura hiyo.
Hasina ambaye yupo uhamishoni India nayo alikashifu uchaguzi huo akisema kuwa chama chake kuzuiwa ni ukiukaji wa demokrasia.
“Tunatao wito matokeo ya uchaguzi huu yafutiliwe mbali kwa sababu haukuwa wa haki, haukuzingatia katiba na haki za Awami League zilikiukwa kwa kuzuiwa kushiriki uchaguzi,” akasema Hasina akiwa uhamishoni
Kinaya ni kwamba katika utawala wake, alikuwa na mazoea ya kuvikandamiza vyama vya upinzani.