Dondoo

Maombi yamfanya polo mchepukaji kuanika ‘mipango’ yake kwa mkewe

Na KALUME KAZUNGU April 16th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAVUENI, Kilifi:

KALAMENI ambaye kwa muda mrefu amekuwa akimtesa mkewe kijijini hapa kupitia uzinzi, amejipata akichanganyikiwa kwa kile kinachoaminika kuwa ni maombi ya mwanadada huyo.

Kwa karibu miaka kumi sasa tangu waoane, jamaa amekuwa mtu wa mipango mingi ya kando, hali ambayo imekuwa ikimkondesha mkewe.

Kila wakati mwanadada alipojaribu kumkanya, jamaa aliruka na kumtolea macho kwa ukali.

Mkewe aliafikia kukimbilia usaidizi wa Mungu, ambapo alianza kufunga na kuomba ili Mola amgeuze mume huyo wa tabia mbaya.

Wiki jana, jamaa alianza kuchanganyikiwa kwani kila mara mipango wake wa kando wanapompigia simu amekuwa akijipata akikimbiza simu hizo kwa mkewe na kumwagiza azipokee.