Jombi mashakani siri ya miezi sita kwa mkewe kuhusu hela zake benki ikifichuka kiajali
RUIRU Mjini:
JOMBI mmoja mjini hapa, alizua kicheko baada ya kufichua kuwa kwa miezi sita alikuwa akimdanganya mkewe kuhusu mshahara wake.
Kila mwisho wa mwezi, alimwambia amelipwa nusu ya kiasi halisi akidai kampuni yao ina matatizo ya kifedha. Lengo lake lilikuwa kujiwekea akiba ya siri ili kununua pikipiki.
Lakini siri ilifichuka siku alipolegea na kusahau kubadili ujumbe wa benki uliokuwa ukionyesha kiasi kamili cha hela alichohifadhi.
Mkewe alipoona ujumbe huo, alishtuka na kumkabili papo hapo. Kilichofuata ni mjadala mkali nusura uvutie majirani.
Jamaa alijitetea akisema alitaka “kusurprise” familia, lakini mkewe alidai huo ni usaliti wa kifedha.
Mwishowe, waliamua pesa hizo zitumike kulipa madeni ya nyumba badala ya kununua pikipiki.