Dimba

Kenya Police Bullets mabingwa KWPL

Na TOTO AREGE May 10th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

Kenya Police Bullets ndio mabingwa wa Ligi kuu ya Wanawake (KWPL) msimu huyu wa 2025/26.

Bullets ya kocha David Bujego, imechukua ubingwa huo mara tatu mtawalia sasa (2023/24 na 2025/25 wakati huo ikinolewa na Beldine Odemba ambaye aliondoka mwishoni mwa msimu jana).

Washikadoria hao walijihakikishia ubingwa, baada ya ushindi finyu wa 1-0 dhidi ya Trinity Starlets jana, katika uwanja wa Trinity Complex mjini Gilgil Kaunti ya Nakuru leo. Bao hilo la pekee lilifungwa na mshambuliaji raia wa Uganda Margaret Kunihira dakika ya 40 ya mchezo.

Bao hilo lilikuwa la 14 la Kunihira msimu huu, akiwa anaongoza jedwali la wafungaji bora kutoka na mechi 19.

Bullets sasa itawakilisha Kenya katika michuano ya Baraza la Mashirikisho ya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ya kufuzu michuano ya klabu bingwa Afrika nchini Rwanda baadae mwaka huu.

Mara ya kwanza Bullets walishiriki 2024 nchini Ethiopia na wakamaliza nafasi ya pili mwaka jana walimaliza wa tatu katika mashindano yaliyoandaliwa jijini Nairobi.

Ikiwa imesalia mechi moja msimu kukamilika wikendi hii, Bullets wanaongoza jedwali kwa alama 49. Starlets kwa upande mwingine walidondoka hadi nafasi ya tano wakiwa na alama 33.

Katika mechi nyingine, Kibera Soccer Women walimaliza msimu nafasi ya tatu kwa alama 34 baada ya ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Zetecg Sparks. Mabao hayo yalifungwa na Neema Dorcas (2), Amina Nyakoa (32) na Ann Arusi (38).

Mvua ya mabao ilishudiwa katika uwanja wa Mumboha Kaunti ya Vihiga ambapo, mabingwa wa zamani Vihiga Queens walipata ushindi wa 3-0 dhidi ya Gideon Starlets.

Soccer Assassins nao walilala mikononi mwa Kayole Starlets ambao waliwapiga 1-0.

Matokeo ya Jumapili

Trinity Starlets 0-1 Kenya Police Bullets

Zetech Sparks 0-3 Kibera Soccer Women

Soccer Assassins 0-1 Kayole Starlets

Vihiga Queens 3-2 Gideon Starlets