Habari za Kitaifa

Maaskofu walaani matumizi ya wahuni katika siasa

Na JOSEPH KINUTHIA June 23rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MAASKOFU wa Kanisa Katoliki Kenya (KCCB) wametoa onyo kali kuhusu kile wanachokiita kuongezeka kwa “wahuni wanaolindwa na watu wenye ushawishi” katika maisha ya kisiasa na kijamii nchini, likisema mwenendo huo unadhoofisha demokrasia, kueneza hofu na kuhalalisha vurugu.

Katika taarifa kali ya Hali ya Taifa iliyotolewa Karen, Nairobi, maaskofu hao walisema kuongezeka kwa makundi ya kulipwa kuvuruga mikutano, kutisha wapinzani na kuwatia hofu wananchi ni mwelekeo hatari ambao lazima ukabiliwe haraka.

Wameonya kuwa matumizi ya magenge ya kukodi kuvuruga mikutano ya hadhara, mikutano ya kisiasa na shughuli za kiraia yanaweza kugeuza mchakato wa kidemokrasia kuwa uwanja wa vitisho badala ya uhuru wa kujieleza.

Maaskofu hao walisema wana wasiwasi kuwa makundi hayo yanazidi kuhusishwa na watu wenye ushawishi mkubwa, hali wanayosema inachochea ukosefu wa uwajibikaji na kuwaweka vijana katika hatari ya kutumiwa katika uhalifu.