Mheshimiwa akodi nyumba ya siri kuwatumbuiza ‘Maben Ten’
NAIROBI Mjini
KIONGOZI mmoja mwanamke anatikisa vichwa vya watu baada ya kuibuka madai kuwa ana nyumba ya siri ambako hujisitiri na vijana wa kiume.
Inasemekana nyumba hiyo imekodishwa kwa jina la mmoja wa wasaidizi wake ili kuficha umiliki wake halisi.
Ili kuepuka kuvutia macho ya umma, ripoti zasema mwanasiasa huyo hujiendeshea gari lake binafsi badala ya msafara wake rasmi anapoelekea huko, hasa usiku.
Mpekuzi wetu anasema kila anapozuru nyumba hiyo, mwanasiasa huyo huwasili akiwa ameandamana na kijana mmoja na kukaa humo kwa saa tatu hadi nne kabla ya kuondoka.
Pia kuna madai kuwa baadhi ya vijana hao anaoburudika nao huenda ni wafanyakazi wake wa ngazi za chini.
Majirani wake sasa wasema huenda wakalazimika kuanika uozo huo kwa kuwa anabadilisha vijana hao kama nguo.
Wengine wamelalama huenda akahatarisha maisha ya vijana hao kwa kuwaambukiza maradhu hatari.