Demu asherehekea mume kumpa pin zake zote za benki na M-Pesa
KIPUSA wa hapa aliweka wazi furaha yake mbele ya shoga zake mumewe alipomfichulia nambari za siri za akaunti zake mbalimbali ikiwemo ya M-Pesa.
Inasemekana jombi alikuwa msiri kama kaburi na mkewe hakujua mengi kumhusu lakini juzi mambo yalibadilika.
“Dharura ilitokea jamaa akaugua ghafla na kupoteza uwezo wa kunena. Mke alikopa pesa na kumtafutia matibabu hadi akapona,” mdaku akaarifu.
Hali yake ilipokuwa shwari jombi alimpa mke nambari zote za siri akisema ameona umuhimu awe nazo.
“Sasa nina nambari ya siri ya mpesa na ya akaunti yake ya benki. Ninafurahi ameniamini,” kidosho akasema akiwa na warembo wenzake.