Dimba

Kikosi kitakachowasilisha Kenya WAFCON chatajwa

Na TOTO AREGE July 11th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

Kocha wa Harambee Starlets, Beldine Odemba jana, alitaja kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 kitakachowakilisha Kenya katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) itakayoandaliwa Morocco kuanzia Julai 27 hadi Agosti 16.

Michuano hiyo pia itatumika kama njia ya kufuzu Kombe la Dunia la Wanawake 2027 litakalofanyika Brazil.

Kenya imepangwa Kundi A pamoja na wenyeji Morocco, Senegal na Algeria. Starlets itaanza kampeni dhidi ya Morocco Julai 26, kabla ya kukutana na Senegal Julai 30 na kumaliza hatua ya makundi dhidi ya Algeria Agosti 2.

Kikosi hicho kimekuwa kambini kwa zaidi ya wiki mbili kikifanya mazoezi Kasarani Annex, Nairobi, na kinatarajiwa kuelekea Miramas, Ufaransa kwa kambi ya mwisho kabla ya kuingia Morocco.

Kikosi cha mwisho

Walinda lango: Lilian Awuor, Annedy Kundu, Vivian Shiyonzo.

Mabeki: Ruth Ingosi, Norah Ann, Elizabeth Ochaka, Euphrasier Shilwatso, Vivian Nasaka, Leah Andiema, Enez Mango, Mary Thambi.

Viungo: Mwanalima Adam, Fasila Adhiambo, Martha Amunyolete, Mercy Airo, Airin Madalina, Terry Engesha, Lorna Nyarinda.

Washambuliaji: Eglay Mukhwana, Shirleen Opisa, Marion Serenge, Valerie Nekesa, Violet Nanjala.