• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
“Nilikasirika sana nilipofungiwa nje ya ndege ya mauti Ethiopia’

“Nilikasirika sana nilipofungiwa nje ya ndege ya mauti Ethiopia’

Na LEONARD ONYANGO

KUCHELEWA kwa dakika mbili pekee kulimfanya raia wa Ugiriki kunusurika kifo katika ajali ya ndege iliyosababisha vifo vya watu 157.

Antonis Mavropoulos, sasa angekuwa mwathiriwa wa 158, endapo angewasili mapema na kuabiri ndege hiyo.

Ndege hiyo aina ya Boeing 737-800 MAX iliondoka jijini Addis Ababa saa 2:38 asubuhi na kupoteza mwelekeo dakika sita baadaye. Ilianguka karibu na mji wa Bishoftu takribani kilomita 60 kutoka Addis Ababa.

“Nilikasirika sana nilipofika katika lango nikakuta limefungwa na hakukuwa na mtu wa kunisaidia,” akasema Mavropoulos kupitia mtandao wa Facebook ambapo ameweka picha ya tiketi yake.

Mavropoulos, ambaye ni rais wa shirika la International Solid Waste Association, alikuwa akielekea Nairobi kuhudhuria mkutano wa kila mwaka wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), kulingana na shirika la habari la Ugiriki, Athens News Agency.

“Nilipelekwa katika kituo cha polisi kilichoko katika uwanja wa ndege. Afisa wa polisi aliniambia niwe mpole na kuomba Mungu kwa sababu sikupanda ndege hiyo,” akasema Mavropoulos.

Polisi walimzuilia kwa muda wakimhoji ni kwa nini hakupanda ndege hiyo iliyopata ajali: “Walisema hawangeweza kuniachilia huru kabla ya kunihoji na kujua sababu yangu kukosa kupanda ndege iliyoanguka,” akasema.

Wakati huo huo, mkazi wa Dubai, Ahmed Khalid pia ameelezea furaha yake huku akidai kuwa alifaa kuabiri ndege iliyopata ajali.

Alifaa kuabiri ndege ya kuunganisha lakini akaabiri mbadala alipopata ndege iliyoanguka ikiwa imeondoka.

You can share this post!

Majonzi, vilio baada ya ajali ya ndege Ethiopia

Yakujuzu kufahamu haya kuhusu kilimo cha tufaa

adminleo