• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 4:25 PM
Kasisi Mkenya achaguliwa askofu wa Kianglikana New Zealand

Kasisi Mkenya achaguliwa askofu wa Kianglikana New Zealand

CHARLES WASONGA na MASHIRIKA

KASISI Mkenya, Steve Maina, amechaguliwa kuwa Askofu Mpya wa Kanisa la Kianglikana katika jiji la Nelson, nchini New Zealand.

Maina alitawazwa kuwa kasisi mnamo mwaka wa 2004 baada ya kuhudumu katika matawi kadha ya Kianglikana katika Kaunti ya Nairobi.

Kwenye taarifa iliyochapishwa kwenye vyombo vya habari nchini New Zealand, maaskofu wakuu wa Kanisa la Kianglikana katika madayosisi ya Aoteorea na Polynesi waliommiminia sifa Bw Maina walimtaja kama mtumishi ambaye amekuwa akihudumu kwa bidii na kujitolea.

“Steve analeta huduma yenye mwelekeo katika nyanja zote na anaheshimiwa kwa bidii na kujitolea kwake kuendeleza injili,” wakasema Maaskofu hao wakuu.

Waliongeza kuwa uongozi wake uongozi wa Maina amewasaidia vijana na watu wengi ambao amewahi kuwahudumia.

“Steve analeta moyo wa utumishi na fikra nzuri katika yale yote anayofanya katika kanisa hili, wakasema.

Maina ambaye alizaliwa mnamo 1970 atachukua mahala pa Richard Ellena, atakapotawazwa rasmi.

“Nimefurahi kwa kuchaguliwa kwa wadhifa huu na ninaukubali kwa unyenyekevu,” akasema.

“Je, mtoto wa Afrika anaweza kuchaguliwa? Mtu kutoka Kenya? Niko na hamu ya kuhudumu,” Bw Maina akaendelea kusema.

You can share this post!

NJAA: Mito na maziwa yakauka Baringo na Nakuru miti...

Hofu sanamu ya Yesu kutiririkwa na machozi ya damu

adminleo