• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Raia wa Uganda waliolemewa kulipa hoteli kusukumwa ndani

Raia wa Uganda waliolemewa kulipa hoteli kusukumwa ndani

Na RICHARD MUNGUTI

RAIA wawili wa Uganda Alhamisi walioshindwa kulipa gharama ya malazi katika hoteli moja jijiji Nairobi sasa watalala katika gereza la Viwandani, Nairobi miezi sita wakishindwa kulipa faini ya Sh20,000 kila mmoja.

Mzee Sebowa Kiboigo mwenye umri wa miaka 72 alisababisha kicheko mahakamani aliposema, “Tangu enzi za hayati marais Milton Obote na Idd Amin na hata sasa wakati wa utawala wa Rais Yoweri Museveni nchi ya Kenya imekuwa nzuri kwa raia wote wa Uganda.”

Bw Kiboigo aliyeshtakiwa pamoja na mpwawe Mathias Mgemeso mwenye umri wa miaka 27 alimweleza hakimu mwandamizi Bw Peter Ooko kuwa ameishi Kenya miaka 40 akifanya biashara za kununua vinyango na kuziuza Marekani na hajawahi fikishwa kortini.”

Akasema, “angu miaka ya 1970 nimekuwa nikifanya kazi nchini Kenya. Nchi hii imekuwa nzuri kwa raia wa Uganda n ahata nyakati machafuko na kisiasa yalipokumba nchi yetu Uganda , Kenya ilitupokea na kutupa kazi za Ualimu , Udaktari na kazi za viwandani.”

Alisema yeye ni Mhandisi wa Masuala ya Kemikali na amekuwa akiishi Kenya tangu alipohitimu masomo yake nchini Amerika miaka ya 1970.

Huku akisakata densi akiwa mchangamfu na mwenye furaha kwa kuruhusiwa kuzugumza mahakamani, Kiboigo alisema hakuwa na pesa za kulipa Comfort Hotel alikolala siku nne.

“Nawashukuru wasimamizi wa wa hoteli ya Comfort kwa kunielewa hata kunipeleka katika benki ya Chase Bank ambapo pesa zangu zimeshikwa baada ya kuwekwa chini ya mrasimu wa Serikali,” Bw Kiboigo alimweleza hakimu.

Aliongeza kusema kuwa ametumiwa pesa kupitia Benki ya Western Union na ndugu yake na sasa “niko tayari kulipa hoteli hiyo.”

Mzee huyo alieleza mahakama kuwa umri wake wa miaka 72 haumruhusu kufanya ukora wa njia yoyote ile.

Karani wa mahakama awasomea mashtaka washukiwa mbele ya hakimu Peter Ooko. Picha/ Richard Munguti

Alikiri maelezo ya kiongozi wa mashtaka Bi Celestine Oluoch kuwa kati ya Machi 10 na Machi 19 alikuwa amekodisha chumba cha kulala akiwa na mwanawe.

“Mshtakiwa alitoroka hoteli hiyo bila kulipa lakini akarudi tena Machi 18 na 19 na kupokewa kwa mikono miwili lakini akashtakiwa aliposhindwa kulipa ada ya malazi,” alisema Bi Oluoch.

Mshtakiwa huyo alieleza korti hana la kusema ila kushukuru nchi ya Kenya kwa kumpa makao kwa zaidi ya miaka 40 lakini akadokeza kufilisika kwa benki ya Chase Bank kulimfanya akumbane na makali ya sheria.

Mshtakiwa huyo aliomba msamaha na kusema hangelipenda kuchokoza nchi hii ambayo inaishi na amani na majirani wake.

“Mimi sisemi eti mimi ni mtu mtakatifu nisiye na udhaifu. La hasha. Mimi ni binadamu kama wengine walio na udhaifu kama huu ambao umenifanya kufika mahakamani nikiwa na umri mkubwa,” alisema mshtakiwa.

Aliongeza kusema kwa maisha yake hapendelei watu wanaowalaumu watu wakifanya makosa hata ikiwa wako na umri wa miaka 10.Mtu anaweza kufanya makosa wakati wowote.

“Ulikuja Kenya kufanya nini?” Bw Ooko alimwuliza Mzee huyo.

“Nilikuwa nimemleta mpwa wangu kutembea katika soko ya Maasai kununua ushanga,” Kiboigo alitoboa siri.

Akaendelea, “Mpwa wangu ameanza kuuza ushanga ng’ambo na nilikuwa nimemleta kumtembeza aone kule zinatengenezwa na kuuzwa. Miaka yangu yote nikiishi Kenya nilikuwa nauza vinyango na vikapu nchini Amerika. Nilipata ufanisi mkubwa na pesa zangu nilikuwa naziweka katika benki ya Chase Bank.”

Bw Kiboigo aliendelea kusema wasimamizi wa benki hii iliyowekwa chini ya mrasimu kutoka Benki Kuu ya Kenya (CBK) walimwandikia barua pepe na kumtaka awasilishe pasi yake ya kusafiri na kitambulisho ndipo pesa zake zilipwe.

You can share this post!

Njaa mahindi yakioza

Uchangamfu KWS kutangaza mbuga kwa picha ya vifaru...

adminleo