• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Kenya yaona vimulimuli tenisi ya Afrika Mashariki

Kenya yaona vimulimuli tenisi ya Afrika Mashariki

Na GEOFFREY ANENE

KENYA ilianza kampeni yake katika mashindano ya tenisi ya Afrika Mashariki vibaya baada ya kupoteza kwa mechi 3-0 dhidi ya Burundi jijini Kigali, Rwanda, Jumapili.

Katika kitengo cha mchezaji mmoja mmoja cha wavulana wasiozidi umri wa miaka 12, Liberty Baraka Kibue alipepetwa 6-2, 6-1 na Abdoul Shakur Malick naye Raqeem Virani akazabwa 6-0, 6-3 na Abdilah Ndayishimiye.

Ushirikiano wa Malick na Ndayishimiye pia uliwazidi Kibue na Virani nguvu 6-1, 6-3.

Wawakilishi wa Kenya katika kitengo cha wasichana wasiozidi umri wa miaka 12, Anouk Vandevelde, Reha Kipsang’ na Debbie Polo wataingia uwanjani Jumatatu kukabiliana na wenyeji Rwanda. Timu ya Kenya inanolewa na Caroline Oduor.

Mataifa manne yanashiriki mashindano haya. Mbali na Kenya, Rwanda na Burundi, Uganda pia inashiriki. Tanzania ilijiondoa dakika ya mwisho kutokana na ukosefu wa udhamini.

Mashindano haya yalianza Machi 4 na yatakamilika Machi 8, 2018.

You can share this post!

Hatimaye Nzoia yaonja ushindi KPL

Ndoto ya Birgen kushindia Kenya medali yatimia

adminleo