• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 11:55 AM
Hakimu aamuru anayedaiwa kuiba kioo apelekwe hospitalini kutibiwa nyeti zilizoumizwa akikamatwa

Hakimu aamuru anayedaiwa kuiba kioo apelekwe hospitalini kutibiwa nyeti zilizoumizwa akikamatwa

Joseph Odero Olanjo akiwa kortini Jumatatu aliposhtakiwa wizi wa kioo cha gari la makavazi ya kitaifa- Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

HAKIMU Mkuu katika Mahakama ya Milimani Nairobi Francis Andayi ,  Jumatatu alimwamuru afisa mkuu wa polisi katika mahakama hiyo ampeleke mshukiwa hospitali kutibiwa nyeti zake baada ya kuungama alivutwa yeti zake na walinzi waliomshika akiwa na kioo cha gari la makavazi ya kitaifa.

“Mheshimiwa naumia sana. Naumwa na dhakari yangu. Sehemu yote ya eneo la nyeti zangu inauma. Nilivutwa mboo yangu na mabawabu walionishika, naomba uamuru nipelekwe hospitali,” aliomba Joseph Odero Olanjo.

Olanjo aliendelea, “Mbali na yeti zangu, natokwa na damu pua la kushoto. Niliumizwa vibaya. Naomba nipelekwe hospitali.”

Mshtakiwa huyo pia alimsihi hakimu aamuru atibiwe kidole cha kati cha mkono wake wa kulia kilichokeketwa kwa wembe na askari waliomtia nguvuni.

Akasema , “Unavyoniona nimesimama mbele yako mimi naumwa na kila kiungo mwilini mwangu. Naomba uamuru nitibiwe.”

Bw Andayi aliamuru afisa msimamizi wa idara ya polisi mahakamani ampeleke hospitali.

Olanjo alishtakiwa kwa wizi wa kioo chenye thamani ya Sh40,000 cha gari la Makavazi ya Kitaifa mnamo Machi 1, 2018.

You can share this post!

Taabani kwa kukosa kulipia ngozi ushuru

Mshukiwa wa ugaidi kusalia ndani hadi kesi iamuliwe

adminleo