• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Mwanamke aliyeshiriki ngono na mtoto aungama ana Ukimwi

Mwanamke aliyeshiriki ngono na mtoto aungama ana Ukimwi

Na TITUS OMINDE

MWANAMKE mwenye umri wa miaka 24 anayekabiliwa na kesi ya kuishi na kushiriki mapenzi na kijana wa umri wa miaka 15 ameeleza mahakama moja mjini Eldoret kwamba yeye ni hawara na anaugua ugonjwa wa Ukimwi.

Akitoa ushahidi mahakamani, mwanamke huyo alisema kwamba wamekuwa wakitumia kinga kila mara wanaposhiriki mapenzi na kukana kuambukiza kijana huyo ugonjwa.

“Naam, ni kweli tumekuwa tukiishi naye kama mke na mume japo mimi ni hawara hapa mjini Eldoret. Kila tunaposhiriki huba huwa hatukosi kutumia kinga kwa sababu mimi nina utu na namjali sana mpenzi wangu,” akasema mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Eldoret Bi Naomi Wanjiru.

Kulingana na ripoti ya uchunguzi wa madaktari kutoka Hospitali ya Moi Eldoret, mwanamke huyo alipatikana na virusi vya ugonjwa wa ukimwi huku hali ya mpenziwe ikikosa kuwekwa wazi.

Wazazi wa kijana huyo waliripoti kutoroka kwa mwanao kutoka nyumbani tarehe 6 mwezi Disemba mwaka jana katika kituo cha polisi cha Kiambaa.

Siku nne baadaye polisi walimfumania akiwa na mpenziwe kwenye nyumba moja ya kukodisha viungani mwa mji wa Eldoret.

Alipofikishwa mahakamani mbele ya hakimu mkazi huyo, mwanamke husika aliyakana mashtaka ya kuishi na kushiriki ngono na mpenzi ambaye hajahitimu umri wa 18.

Bi Wanjiru aliratibisha kusikizwa kwa kesi hiyo tarehe 21 mwezi huu ambapo atatoa mwelekeo zaidi.

 

You can share this post!

Ni usaliti mkubwa Raila kukutana na Uhuru – Miguna...

Kalameni aliyezaa na dada apanga kumuoa

adminleo