• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 2:13 PM
Mpaka kati ya Rwanda na Uganda wafunguliwa

Mpaka kati ya Rwanda na Uganda wafunguliwa

Na AFP

SERIKALI ya Rwanda hatimaye imefungua mpaka wake na Uganda katika eneo la Gatuna ili kuruhusu magari yanayobeba bidhaa kupita na pia biashara kati ya mataifa hayo kurejelewa.

Mpaka huo ulifungwa miezi mitatu iliyopita kutokana na uhasama kati ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Paul Kagame wa Rwanda, na umeathiri shughuli za kibiashara na maisha ya raia wengi wa mataifa hayo mawili.

Hata hivyo, Rwanda ilijitetea kwamba ilifunga mpaka huo ili kupisha ukarabati wa miundombinu na ikakanusha kwamba uamuzi wake ulichochewa na tofauti za kisiasa kati ya viongozi wa mataifa hayo mawili.

Marekebisho

Serikali ya Rwanda pia imesema mpaka huo umefunguliwa upya ili ukaguliwe na kuona iwapo marekebisho yaliyotekelezwa yamerahisisha usafirishaji wa bidhaa.

Uganda imekuwa ikidai Rwanda imetuma majasusi kuchunguza serikali yake, nayo serikali ya Rais Kagame inalalamika kwamba raia wake wamekuwa wakipigwa na kunyanyaswa mpakani na polisi kutoka Uganda.

You can share this post!

VIDUBWASHA: Mbali na wakati, itakujuza matokeo ya soka pia...

Manchester United wasaka kizibo cha Pogba

adminleo