• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 2:10 PM
Kutuny, Kamanda na Moses Kuria wapinga uteuzi wa Mariga

Kutuny, Kamanda na Moses Kuria wapinga uteuzi wa Mariga

Na Samwel Owino

UTEUZI wa McDonald Mariga kupeperusha bendera ya chama cha Jubilee katika uchaguzi mdogo wa Kibra unaendelea kukumbwa na upinzani ndani ya chama hicho, Mbunge wa Cherangany Joshua Kutuny akiwa wa hivi punde kuupinga.

Mbunge huyo jana alisema mfumo ambao Bodi ya Kitaifa ya Uchaguzi (NEB) ya chama hicho ulitumia kumteua mwanasoka huyo wa kimataifa Jumatatu unahujumu demokrasia.

Akiongea katika Majengo ya Bunge, Nairobi, Bw Kutuny alisema alitarajia kwamba bodi hiyo ingehakikisha wagombeaji wote 16 wamepigiwa kura ya moja kwa moja na wanachama wa Jubilee.

“Siasa haitambui jina kubwa, tunahitaji kujisaili upya na kuhakikisha tumerekebisha mambo katika nyumba yetu. Uteuzi ulipasa kufanya kwa njia ya upigaji kura kwa sababu hiyo ndio mbinu ya kipekee ambayo itahakikisha chama chetu kinawasilisha mgombeaji bora,” akaeleza.

Wengine ambao wamepinga uteuzi huo, uliotangazwa na mwenyekiti wa NEB Andrew Musangi, ni mbunge maalum Maina Kamanda na Moses Kuria (Gatundu Kusini).

 

You can share this post!

Dalili kaunti inavunja urafiki na Ruto

Lusaka awataka viongozi waeleze faida ya miswada

adminleo