• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 PM
KAULI YA WALIBORA: Kiswahili kitakwezwa tu kupitia ari na juhudi za wasemaji wake

KAULI YA WALIBORA: Kiswahili kitakwezwa tu kupitia ari na juhudi za wasemaji wake

Na PROF KEN WALIBORA

Mhakiki wa Kinaijeria Obi Wali aliwahi kuuliza: “Kiingereza kingekuwa wapi kama waandishi wa Kiingereza wangeamua kuandika kwa lugha za Kifaransa au Kilatini, lugha ambazo zilikuwa na hadhi zamani zile kuliko Kiingereza?” Obi Wali alilalamikia kudhalilishwa kwa waandishi wa Kiafrika waliozitumia lugha za Kiafrika.

Kilichochochea kauli ya Obi Wali ni kongomano la fasihi ya Kiafrika lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Makerere, 1962.

Wali alilalamika ni kwa nini waandishi wanaoandika kwa lugha za Kiafrika hawakualikwa kwenye kongomano. Mnamo 1986, Mkenya Ngugi wa Thiong’o aliandika katika kitabu, Decolonising the Mind, kwamba yeye alikuwa ameandika hadithi fupi mbili tu kwa Kiingereza nazo zilitosha kufanya aalikwe.

Nani walioachwa nje? Ni waandishi wakongwe na wabobezi wa lugha za Kiafrika kama vile Fagunwa aliyeandikwa kwa Kiyoruba na Shaaban bin Robert aliyeandika kwa Kiswahili.

Mhakiki wa Kinaijeria Obi Wali aliwahi kuuliza: “Kiingereza kingekuwa wapi kama waandishi wa Kiingereza wangeamua kuandika kwa lugha za Kifaransa au Kilatini, lugha ambazo zilikuwa na hadhi zamani zile kuliko Kiingereza?” Obi Wali alilalamikia kudhalilishwa kwa waandishi wa Kiafrika waliozitumia lugha za Kiafrika.

 

Sababu ya kutoalikwa 

Kilichochochea kauli ya Obi Wali ni kongomano la fasihi ya Kiafrika lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Makerere, 1962. Wali alilalamika ni kwa nini waandishi wanaoandika kwa lugha za Kiafrika hawakualikwa kwenye kongomano.

Mnamo 1986, Mkenya Ngugi wa Thiong’o aliandika katika kitabu, Decolonising the Mind, kwamba yeye alikuwa ameandika hadithi fupi mbili tu kwa Kiingereza nazo zilitosha kufanya aalikwe.

Nani walioachwa nje? Ni waandishi wakongwe na wabobezi wa lugha za Kiafrika kama vile Fagunwa aliyeandikwa kwa Kiyoruba na Shaaban bin Robert aliyeandika kwa Kiswahili.

Turejelee kauli ya Obi Wali: Kiingereza kingekuwa wapi kama waandishi wa Kiingereza wangeamua kuandika kwa lugha za Kifaransa au Kilatini ambazo zilikuwa na hadhi kubwa zaidi kuliko Kiingereza zamani zile? Kiingereza kingekuwa wapi kama William Shakespeare na Charles Dickens wangeandika kwa lugha isiyokuwa yao?

Hili ni swali kuhusu kile ambacho kingetokea ingawa kwa kweli hakikutokea. Nini hasa kilichotokea basi? Kwanza lugha iliyoonekana kuwa ya washenzi, ya makabwela, na walalahoi iliinuka ikakwea sana kwa juhudi za wasemaji wake kujitolea mhanga kuitumia.

Hii leo lugha hii ya Kiingereza iliyokuwa lugha ya washenzi, ndicho Kiswahili cha dunia, chambilecho rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, yaani lugha ya dunia.

 

Lugha ya wachache

Nini kingetokea? Isingekuwa lugha hii ya Washenzi imekua na kunawiri kwa kadiri kubwa namna hiyo. Ingekuwa lugha ya watu wachache katika kisiwa kidogo kiitwacho England au Uingereza.

Kiingereza kingekuwa lugha isiyokuwa na maandishi mengi maarufu kama kilivyo Kiibo cha Chinua Achebe. Kiibo cha Achebe hakijulikani sana wala hakijatumiwa sana katika maandishi.

Achebe mwenyewe alidai kwamba kapewa Kiingereza na kwamba hiyo alikuwa hana budi kukitumia. Naye alikitumia sana katika maandishi yake. Alikitajirisha Kiingereza na kutoa mchango unaofanana na ule Shakespeare na Dickens kwa kadiri fulani.

Aliwafanyia kazi yao ya kukikweza Kiingereza na kukifanya lugha ya dunia. Waingereza hao walipokufa walikuwa na  deni la kukikuza na kukweza Kiibo cha Achebe.Mbona hali kama  hii inatokea ya Waingereza kusaidiwa na wengine?

Hao wengine, kama Achebe, wana lugha zao, lakini hayamkiniki kupata msaada  wa Waingereza kuzikweza lugha zao.  Kisa na maana?  Waingereza walitiisha maeneo mengi ya dunia na kuyafanya makoloni.   Ushawishi wao wa kikoloni bado ungalipo mpaka leo.

 

Prof. Ken Walibora ni msomi wa fasihi, mwanahabari na mwandishi mtajika katika ulimwengu wa Kiswahili.

You can share this post!

GWIJI WA WIKI: Timothy Kinoti M’Ngaruthi

KAULI YA MATUNDURA: Mkangi aliandika Walenisi kwa mafumbo...

adminleo