• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Msomi mashuhuri Mkenya afariki

Msomi mashuhuri Mkenya afariki

Na KITAVI MUTUA

ULIMWENGU Jumatatu uliomboleza kifo cha profesa wa masuala ya kidini, John Samuel Mbiti ambaye alikuwa maarufu kimataifa.

Prof Mbiti alifariki akiwa na umri wa miaka 88 mnamo Jumapili alipokuwa akitibiwa mjini Bergdorf, Uswizi ambako alikuwa akiishi kwa miongo mingi.

Alipata umaarufu kimataifa wakati alipoandika kitabu chake cha kwanza cha African Religions and Philosophy ambacho kilichapishwa mnamo 1969.

Katika kitabu hicho, alitilia shaka misimamo ya Kikristo kwamba dini na imani za Kiafrika ni za kishetani.

Prof Mbiti alikuwa kasisi wa Kanisa la Anglikana na alizaliwa katika eneo la Mulango, Kaunti ya Kitui.

Alikuwa mfasaha wa lugha ya Kigiriki ambayo ni mojawapo ya lugha za kwanza asili zilizotumiwa kuandika Biblia.

Marehemu alitumia miaka 12 ya uzeeni mwake kuanzia 2003 hadi 2015 kutafsiri Biblia asili ya Kigiriki kwa Kikamba ambapo alikosoa zaidi ya maneno 1,000 aliyosema yalitafsiriwa kimakosa katika Biblia.

You can share this post!

Korti yaagiza ukaguzi KTDA baada ya kilio cha wakulima

Lusaka aonya MCAs dhidi ya kupapia kurekebisha Katiba

adminleo