• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Aibu ya mashirika kulipa walinzi Sh4,000

Aibu ya mashirika kulipa walinzi Sh4,000

NA MARY WAMBUI

IMEBAINIKA kuwa mashirika mengi ya kiserikali huwalipa walinzi wa kibinafsi mshahara wa chini ya Sh27,000 ilhali kiwango kinachopendekezwa kisheria kinazidi kiasi hicho.

Kwa wastani, mashirika ya serikali ambayo yalitoa kandarasi kwa kampuni zinazotoa huduma za ulinzi, mara nyingi hulipa kila mlinzi kati ya Sh13,000 hadi Sh27,840 kwa mwezi.

Baada ya makato mengi kwenye pesa wanazolipwa, imebainika walinzi wengi huishia kutia mfukoni Sh4,000 pekee.

Hata hivyo, mashirika ya NCPB, KPLC, KR na KPLC ni kati ya yale yanayolipa vizuri, hii ikiwa ni Sh27,840, Sh26,100, Sh24,844 na Sh24,360 mtawalia.

Walinzi katika Shule ya Upili ya St Thomas Acquinas, Kitui, St Monica Girls Kitui, Shirika la Nyayo Tea Zone na Chuo Kikuu cha JKUAT ndio hulipwa vibaya kwa kuwa kila mwezi wao hupata Sh12,000, Sh13,000, Sh14,000 na Sh15,000 mtawalia.

Huku makataa ya kutekelezwa kikamilifu kwa sheria zinazoongoza sekta ya walinzi wa kibinafsi zilizopitishwa na bunge yakikaribia, mashirika haya ya serikali sasa huenda yakakumbatia Shirika la Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS) ambalo hutoa huduma kwa gharama ya chini mno.

Mkurugenzi wa NYS Matilda Sakwa alisema fedha ambazo hulipwa na mashirika ya serikali huelekezwa kwa shirika hilo, hii ikiwa na maana kwamba pesa anazolipwa kila mlinzi huwa haziongezeki.

You can share this post!

SENSA: Kila Mkenya anadaiwa Sh124,000

Maraga adai Ikulu ina njama ya kumng’oa mamlakani

adminleo