• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 3:25 PM
John Baraza sasa kuwaongoza ‘Batoto Ba Mungu’

John Baraza sasa kuwaongoza ‘Batoto Ba Mungu’

Na CHRIS ADUNGO

MCHEZAJI wa zamani wa Harambee Stars John Baraza amepata nafasi ya pili kuongoza kikosi cha Sofapaka baaada ya kocha Sam Ssimbwa kujiuzulu. Taarifa kutoka kwa klabu hiyo imethinitiha haya.

Taarifa hiyo inasema kuwa Baraza, ambaye alipata ufanisi akiichezea ‘Batoto ba Mungu’, atakuwa kocha mkuu wa muda hadi pale klabu hiyo itapata kocha wa kudumu katikati ya msimu.

Baraza, ambaye alishinda ubingwa wa Ligi Kuu ya Kenya mnamo 2009, alichangia pakubwa timu hiyo kuponea 2016 wakati ilipitia wakati mgumu ligini na kupewa nafasi ya naibu kocha mkuu baada ya SSimbwa kuwasili Januari 2017 kutoka Uganda.

“Sofapaka ingependa kutangaza kuwa kocha kutoka Uganda Sam Ssimbwa alijiuzulu akilalamikia matokeo duni ya timu na kulemewa kuiletea ushindi.

“Nafasi ya Ssimbwa itachukuliwa na John Baraza kwa muda, hadi katikati ya msimu ambapo uongozi wa klabu utatathmini matokeo ya timu na kikosi cha ufundi. Baraza amekuwa naibu kocha wa timu hii,” ataarifa hiyo ilisema.

 

 

You can share this post!

Lazima tuzime mashambulizi ya Liverpool, asema Guardiola

Gor kuchuana na Kakamega Homeboyz ‘tarehe...

adminleo