• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Madaktari wa mitishamba wasifu marufuku ya ukataji miti

Madaktari wa mitishamba wasifu marufuku ya ukataji miti

Na TTUS OMINDE

MADAKTARI wa mitishamba kutoka eneo la North Rift wamesifia marufuku ya ukataji miti katika misitu ya umma kote nchini.

Walisema jana kuwa hatua hiyo itasaidia kulinda misitu ambayo ni chanzo cha dawa za kiasili.

Wakiongozwa na daktari Shadrack Moimet wa zahanati ya Koibatek Herbal mjini Elodret, walisema ukataji miti kiholela pia ni tishio kwa tiba za kiasili.

Daktari Moimet alisema marufuku hiyo ya miezi mitatu haitoshi bali yapaswa kuongezwa na kuwa angalau miezi sita.

“Kama daktari wa tiba za kiasili tunapongeza serikali kupitia kwa wizara ya mazingira kwa kupiga marufuku ukataji miti misituni,miti hii ni chanzo kikubwa kwa dawa za kiasili ambazo sisi hutumia kwa kutibu Wakenya,” alisema Dkt Moimet.

Walipongeza waziri wa mazingira Bw Keriako Tobiko huku wakitaka wale ambao wanapinga marufuku hiyo kutilia maanani afya ya Wakenya na mahitaji ya Wakenya kwa jumla pasipokuzingatia tu maswlaa ya biashara yao.

Wakati huo huo madaktari hao walitaka bunge kupitisha sheria kuhusu tiba za kiasili ambao umekuwa bungeni yapata miaka 10 zilizopita.

Dkt Moimet alisema iwapo sheria hiyo itapitishwa itasaidiz kudhibiti sekta ya tiba za kiasili kwa ushirikiano na tiba za kisasa.

 

You can share this post!

Wahadhiri: Tutagoma hadi tupewe haki yetu

Walimu wanaochochea wanafunzi kugoma waonywa

adminleo