• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
Korti yazuia kukamatwa kwa anayehusishwa na picha ya ndege kutoka China

Korti yazuia kukamatwa kwa anayehusishwa na picha ya ndege kutoka China

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA Kuu imezuia kukamatawa na kushtakiwa kwa afisa wa usalama aliyetimuliwa kazini akikabiliwa na tuhuma za kupiga picha ya video ndege ya shirika la Sourthern China iliyowaingiza abiria 239 kutoka nchini China.

Jaji Weldon Korir aliamuru DPP asimkamate na kumshtaki Bw Gire hadi kusikizwa na kuamuliwa kwa kesi aliyoshtaki serikali.

Bw Gire Ali aliwasilisha kesi akipinga kukamatwa na kushtakiwa kwa kurekodi video iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii.

Wakili Danstan Omari aliyewasilisha kesi hiyo katika mahakama kuu amesema Bw Ali alidhulumiwa alipotimuliwa kazini kwa kutekeleza kazi yake ipasavyo.

Katika kesi hiyo, Bw Ali anadai video aliyopiga ilisaidia pakubwa ikitiliwa maanani hofu kuu inayokumba mabilioni ya watu ulimwenguni kutokana na kuzuka kwa maradhi ya Corona ambayo yamesababisha vifo vya maelfu na maelfu ya raia wa China.

Katika kesi aliyowasilisha chini ya sheria za dharura, Bw Ali anaomba mahakama itoe agizo ili asikamatwe na kushtakiwa na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP).

Bw Omari anasema mlalamishi hafai kuchukuliwa alifanya makosa ama kutuhumiwa kuwa tisho kwa vile anatoka eneo la Marsabit.

You can share this post!

Wauguzi wasema hawana uwezo kukabiliana vilivyo na virusi...

Echesa aendelea kuandamwa na madai ya uhalifu

adminleo