• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 9:12 AM
CORONA: Watu kufuatilia mazishi ya wapendwa wao kupitia video mitandaoni

CORONA: Watu kufuatilia mazishi ya wapendwa wao kupitia video mitandaoni

Na MASHIRIKA

KITUO cha Kutafiti na Kudhibiti Maradhi (CDC) nchini Amerika kimewataka watu kuepuka misongamano katika matanga na badala yake kufuatilia mazishi ya wapendwa wao kwa njia ya video.

Wasimamizi wa mochari tayari wamepokea mafunzo kuhusu jinsi ya kuendesha mazishi na kupeperusha hafla hiyo moja kwa moja kwa familia ya mwendazake.

Kituo cha CDC tayari kimeshauri serikali kupiga marufuku mkusanyiko wa zaidi ya watu 50 kwa kipindi cha wiki nane zijazo.

Hiyo inamaanisha kwamba ni watu 50 tu wataruhusiwa kuhudhuria matanga na waliosalia watafuatilia shughuli yamazishi kwa njia ya video kutoka nyumbani.

Hatua hiyo ilifuatia baada ya watu 60 waliohudhuria mazishi katika eneo la Basque, Uhispania kupatikana na virusi vya corona.

You can share this post!

CORONA: Hakuna kwenda kanisani, msikitini

Itumbi na wengine wanne wapoteza kazi katika PSCU

adminleo