• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Nyanya na vitunguu ghali zaidi, viazi na karoti zashuka bei

Nyanya na vitunguu ghali zaidi, viazi na karoti zashuka bei

NA CHARLES MWANIKI

BEI ya vyakula imepanda kwa asilimia 10.6 katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, ikilinganishwa na asilimia 11.6 hapo Aprili na Machi. Hata hivyo, bidhaa za mapishi zimesalia ghali.

“Licha ya hali ya hewa kusalia shwari, bei ya baadhi ya vyakula imekuwa ghali kwa sababu ya changamoto za uchukuzi kutokana na kanuni za kudhibiti Covid-19,” ikasema taarifa kutoka Benki Kuu ya Kenya.

Takwimu kutoka Shiriki la Kitaifa la Takwimu kuhusu mfumuko wa bei zinaonyesha kuwa katika mwezi  wa Mei, vitunguu, nyanya na maharagwe zilirekodi ongezeko kubwa zaidi la bei kwa kilo, huku viazi, kaorti na spinachi zikipungua bei.

Bei ya kilo moja na vitunguu ilipanda kwa asilimia 21.8 mwezi uliopita ikilinganishwa na 2019. Nyanya zilipanda bei kwa asilimia 15.9 huku kilo moja ya maharagwe ikipanda bei kwa asilimia 10.9.

Kwa upande mwingine, karoti zilishuka bei kwa asilimia 22.5, spinachi kwa asilimia 16.8 na viazi kwa asilimia 10.5 ilikinganishwa na mwaka uliopita.

 

You can share this post!

Mswada wa refarenda watua rasmi bungeni

Wakulima wa mtama wapinga ada mpya

adminleo