• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
Niko salama, asema Cherargei

Niko salama, asema Cherargei

Na CHARLES WASONGA

HATIMAYE Seneta wa Nandi Samson Cherargei ameongea kufuatia ripoti zilizosambaa kwamba amehusika katika ajali ya barabarani katika barabara ya Eldoret kwenda Kapsabet usiku wa kuamkia Jumamosi.

Seneta Cherargei alisema yuko “hai na salama” na kuwataka Wakenya kuzingatia masharti ya serikali ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona.

“Niko hai na buheri wa afya. Mungu awabariki nyote. Nawa mikono na make nyumbani. Nawatakia Sabato nzuri,” akasema kupitia akaunti yake ya Twitter.

Ilisemekana kuwa Bw Cherargei alihusika katika ajali ya barabarani katika eneo la Mulango, eneo bunge la Kapseret. Alikuwa ndani ya gari lake aina ya Prado.

Alipata majeraha madogo na kuhudumiwa katika Hospitali ya Kibinafsi ya St Luke, Eldoret, kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.

Siku ya Ijumaa Bw Cherargei alikuwa miongoni mwa viongozi walioandamana na Naibu Rais William Ruto kuhudhuria hafla moja ya kitamaduni eneobunge la Chesumei, kaunti ya Nandi.

You can share this post!

Kisauni Hope FC yawainua vijana

Kafyu kuanza saa tatu usiku

adminleo