• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
Waiguru afika kortini kupinga kutimuliwa kwake

Waiguru afika kortini kupinga kutimuliwa kwake

NA MAUREEN KAKAH

Gavana wa Kaunti ya Kirinyaga Anne Waiguru ameenda kortini kusimamisha kung’olewa kwake mamlakani na madiwani wa kaunti hiyo.

Bi Waiguru alisema kwamba madiwani hao walipuuza amri ya korti kwa sabau korti ilikuwa imesimamisha maswala ya kujadiliana kuhusu kung’atuliwa kwake mamlakani kwa sababu ya janga la corona.

Waiguru aliiomba korti kufutilia mbali kung’olewa kwake mamlakani mpaka kesi hiyo isikizwe.

You can share this post!

Gor Mahia katika mtihani mgumu wa kuhifadhi huduma za...

Mtoto wa miaka 9 afariki baada ya jengo kuporomoka

adminleo