• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:30 PM
LISHE: Jinsi ya kupika maini ya ng’ombe

LISHE: Jinsi ya kupika maini ya ng’ombe

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Dakika 30

Walaji: 4

Vinavyohitajika

• kilo 1 ya maini

• vijiko 4 vya mafuta ya kupikia

• kijiko 1 cha kitunguu saumu

• pilipili mboga mchanganyiko nusu x3

• karoti 1

• nyanya 2

• kitunguu maji 1

• pilipili

• chumvi

• majani ya giligilani

Vinavyohitajika katika kutayarisha maini ya ng’ombe. Picha/ Margaret Maina

Maelekezo

Weka nyanya na pilipili kwenye blenda utengeneze rojo.

Menya, osha na katakata maini.

Katakata kitunguu maji, pilipili mboga na karoti vipande vidogovidogo vya mraba.

Twanga kitunguu saumu na tangawizi.

Katakata majani ya giligilani.

Kwenye sufuria katika moto wa wastani, weka mafuta.

Ongeza kitunguu maji, kitunguu saumu na tangawizi. Kaanga kwa muda wa dakika mbili.

Ongeza maini. Mimina chumvi kiasi.

Endelea kukaanga huku ukigeuzageuza hadi maini yapate rangi ya kahawia kiasi, ila yasiive kabisa.

Ongeza rojo ya nyanya na pilipili. Funika; acha iive kwa moto wa wastani mpaka nyanya ziive vizuri.

Ongeza karoti kasha weka pilipili mboga kwa dakika moja zaidi. Unaweza pia kuongeza maji kidogo ukipenda mchuzi.

Pakua na kiambato utakachopenda na ufurahie.

Maini ya ng’ombe yakiwa tayari yamepikwa. Picha/ Margaret Maina

You can share this post!

Manchester City waponda Burnley na kuchelewesha zaidi...

Elfsborg yatoka sare tasa dhidi ya Helsingborg

adminleo