• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 7:55 AM
Sato Tap, ubunifu wa kisasa wa kunawa mikono

Sato Tap, ubunifu wa kisasa wa kunawa mikono

NA MWANDISHI WETU

Sato, biashara ya kijamii ya Kikundi cha LIXIL kutoka Japan ambayo inakusudia kutatua shida za maji, usafi wa mazingira humu nchini kwa kutoa mifumo ya bei rahisi kwa jamii kote ulimwenguni, imeanzisha mpango wa kunawa mkono kwa jina ‘Sato Tap’.

Kulingana na Hazina ya Watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF), asilimia 40 ya watu ulimwenguni hawana vifaa vya kunawia mikono nyumbani.

Nchini Kenya, asilimia 29 pekee ndio wenye uwezo wa kuishi kwenye mazingira safi, wakati asilimia 41 ya watu hawana maji.

Ili kusuluhisha changamoto hii, LIXIL imetenga Sh100 milioni kusaidia mashirika wa maendeleo ambayo yanaweza kuwasaidia watu milioni 5 kuboresha kunawa mikono.

“Hali ya Covid-19 imezua uhaba mkubwa wa maji, usafi wa mazingira, na usafi kwa jamii barani Afrika na kimataifa. Tunajua kwamba kunawa mikono kwa sabuni ni mojawapo ya hatua madhubuti dhidi ya maambukizi ya magonjwa,” alisema Erin McCusker, Mkuu wa Sato.

“Kwa kuleta muundo na utaalam wa uhandisi wa Sato, pamoja na msaada wa LIXIL, tunakusudia kuharakisha uvumbuzi huu mpya wa mikono kwa soko, na kuifanya iwepo kwa jamii kwa kuimarisha mabadiliko ya usafi.”

Sato ilifanya kazi na washirika wakati wa mchakato wa kubuni, kupokea pembejeo muhimu za kiufundi na kusaidia kuhalalisha ufanisi wa muundo wa Sato Tap unaotumia chupa za plastiki zinazopatikana kwa urahisi.

Sato Tap inaweza kutumika ndani ya nyumba na kama kituo cha kuosha mikono katika maeneo ya umma. Ina ubunifu wa kipekee ambao unapunguza kukaribiana kati ya mtumiaji na bomba, na hivyo kupunguza kuenea kwa magonjwa, wakati inapunguza matumizi ya maji.

Mbali na Sato Tap,ushirikiano uliopo wa LIXIL na UNICEF utapanua shughuli ya kuhakikisha kwamba jamii ina uwezo wa kuwa na mazingira safi.

“Tunajua kuwa njia bora zaidi ya kupunguza kuenea kwa magonjwa ni kunawa mikono. Lakini kwa watoto na familia walio katika mazingira magumu zaidi na hatarishi, hatari ya  Covid-19 inaongezewa na ukosefu wa vifaa vya kunawia mikono, “alisema Kelly Ann Naylor, Mkurugenzi wa UNICEF.

Akihutubu kuhusu umuhimu wa suluhisho la ubunifu wa usafi, Daigo Ishiyama, Afisa Mkuu wa Teknolojia na Masoko katika Sato, alisema Sato Tap itasaidia kuibua mienendo itakayobadilisha maisha.

“Itaimarisha usafi na kuimarisha mabadiliko ya tabia ya kunawa mikono ili kupunguza hatari ya maradhi na kuhifadhi maji. Maoni yetu yanaambatana na Serikali na maoni ya vipaumbele vya Serikali ya Kenya kwa watu wake katika kuimarisha afya, ” alisema.

 

You can share this post!

Mane asahau kupiga goti debi ikianza

Mbunge ataka maafisa wasihujumu uchunguzi chakula...

adminleo