• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 5:22 PM
MAPISHI: Bajia za manjano

MAPISHI: Bajia za manjano

Na DIANA MUTHEU

[email protected]

BAJIA ZA VIAZI (Manjano)

MUDA huu ambapo watu wametulia nyumbani kujikinga dhidi ya maambukizi ya maradhi ya Covid-19, ni vizuri kujitosa jikoni na kujifunza jinsi ya kupika vitafunio ambavyo havihitaji ujuzi mwingi.

Vinavyohitajika

  1. Unga wa bajia (gram flour)
  2. Viazi
  3. Mafuta ya kupika
  4. Maji
  5. Dania
  6. Sufuria nzito/ karai ya kupikia
  7. Chumvi

Maelekezo

Chonga viazi vyako kisha uvikate kwa vipande vyembamba vyenye umbo la duara kisha uviweke kwa sahani au bakuli safi.

Kata dania yako na uweke kwa sahani nyingine.

Katika bakuli nyingine safi, changanya unga wa bajia, chumvi ya kutosha na maji. Hakikisha kuwa mchanganyo huo unashikamana vizuri lakini usiwe mzito sana. Kisha ongeza dania yako na ukoroge vizuri.

Chukua viazi vyako kisha uvimwage ndani ya bakuli iliyo na mchanganyo wa unga, na uchanganye vizuri.

Choma viazi vyako katika mafuta moto.

Pakua na ufurahie.

You can share this post!

Leroy Sane sasa mali rasmi ya Bayern Munich

Kamwe serikali haitaruhusu kamari kurejea –...

adminleo