• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:55 AM
Tembeleeni mbuga zetu, Balala ahimiza Wakenya

Tembeleeni mbuga zetu, Balala ahimiza Wakenya

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Utalii na Wanyamapori, Bw Najib Balala ametoa wito kwa Wakenya kutumia muda huu ambao ada zimepunguzwa kuzuru mbuga za wanyama.

Bw Balala aliwahimiza wananchi kufanya hivyo ili kufurahia urithi wa wanyamapori na kama njia ya kuchochea ukuaji uchumi.

Waziri, hata hivyo, aliwakumbusha wananchi wote kuzingatia kikamilifu masharti yaliyowekwa na Wizara ya Afya ya kuvalia barakoa, kudumisha umbali unaofaa na kuosha mikono au kutumia dawa za kuua viini mara kwa mara ili kukabiliana na janga la COVID-19.

Bw Balala alisema hayo jana alipopokea pikipiki 15 na tairi 180 za magari kama ufadhili kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa Kuhusu Mihadarati na Uhalifu (UNODC), katika makao makuu ya Huduma za Wanyamapori Nchini, Nairobi.

Alieleza kuwa ufadhili huo umejiri wakati ambapo KWS na taifa lote kwa jumla linakabiliana na madhara ya janga la COVID-19, ambalo linasambaratisha mifumo ya kiuchumi duniani.

Mataifa na mashirika yanakabiliwa na changamoto za kupungua kwa mapato na kufanya kuwa vigumu kununua vifaa vya kutosha vya oparesheni za kawaida,” alisema.

You can share this post!

MUTUA: Serikali haijali maslahi ya raia ndani na nje ya nchi

Barakoa na sanitaiza feki zafurika sokoni

adminleo