• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
‘Mke wangu mtamu ila tamaa itaniua…’

‘Mke wangu mtamu ila tamaa itaniua…’

NA PAULINE ONGAJI

“Nimeshindwa kabisa kutulia na mwanamke mmoja kwani licha ya kuwa nimeoa na napata kila kitu mwanamume anahitaji katika uhusiano, bado najipata nikiwa na msukumo wa kurambaramba vya kando.

“Mke wangu ananifanyia kila kitu, na kusema kweli sipangi kumuacha hata siku moja, kumaanisha kwamba nafanya kila niwezalo kulinda penzi letu. Hata hivyo, nimeshindwa kupunguza kiu ya kuwaonja wanawake wengine huko nje.

“Starehe zangu hizi, mimi huzifanya siku na masaa rasmi ya kazi ili mke wangu asije akanishuku.

“Kwa hivyo, japo nina pesa nyingi, vituko vyangu hivi mimi huviendesha jijini Nairobi, na hasa katika maeneo ya haiba ya chini; sehemu ambazo hakuna anayeweza kunishuku.

“Mbali na hayo, kila ninapoagana na binti kukutana mahali fulani, siwezi enda na gari langu, na badala yake mimi hutumia teksi na kuhakikisha kwamba naacha afisini kila kitu kinachonitambulisha.

“Japo nina wapenzi wa kando, naheshimu nyumba na ndoa yangu ambapo sijawahi kumpa mke wangu nafasi ya kutoniamini.

“Na sio kwamba nataka kuridhishwa na yeyote ninayemuonja. Nia yangu ni kutaka kujua tu iwapo nitampata mwanamke mwingine mwenye uzuri sawa na wa mke wangu; kimaumbile, kitabia na hata kimahaba.

“Lakini katika miaka yangu hii yote ya shughuli hii, sijampata hata anayekaribia robo ya wema na uzuri wa mke wangu.

Kwa hivyo nitazidi kutafuta, na hata nikimpata, sio kwamba nitamuoa au kuwa na uhusiano naye. Nia yangu itakuwa kuwaridhisha marafiki zangu wanaoogopa kuoa wakidai wanawake wema hawapo.”

You can share this post!

Lo! si mabinti pekee ‘wachimba migodi’, madume pia...

CHOCHEO: Ni sawa kumwambia mpenzi wako siri zote?

adminleo