• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Polisi Samburu wapata ng’ombe 14 walioibwa

Polisi Samburu wapata ng’ombe 14 walioibwa

FAUSTINE NGILA

POLISI katika Kaunti ya Samburu wameokoa ng’ombe 14 ambao walikuwa wameibwa kutoka eneo la Tiamamut, Kaunti ya Laikipia.

Hiyo inafikisha 27, idadi ya ng’ombe walioibwa na kupatikana kuanzia Juli 25.

Naibu Kamishna wa Kaunti ya Samburu Bw Pius Murugu alisema kwamba ng’ombe hao ni kati ya ngo’mbe walioibwa Laikipia na familia ya washukiwa hao ilikuwa ikitafutwa na maafisa wa polisi.

“Maafisa wa usalama walishirikiana kuokoa ng’ombe 14 ambao ni kati ya ng’ombe 80 walioibwa Tiamamut mwezi uliopita,” alisema Bw Murugu.

Katika soko la Wamba afisa huyo alisema kwamba wanatafuta washukiwa saba ambao wanaaminika kuwa miongozni mwa wezi walioiba ng’ombe katika kaunti jirani.

“Juhudi za kutafuta kama kuna ng’ombe wengine ambao wamefichwa mahali zinaendelea,” alisema.

You can share this post!

Kingi aahidi kuadhibu waliomumunya mamilioni ya corona

Warejeshewa hela zao baada ya corona kutatiza maonyesho