• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Buda amwachia mke uwanja agawe uroda anavyotaka, bila bughudha

Buda amwachia mke uwanja agawe uroda anavyotaka, bila bughudha

Na TOBBIE WEKESA

NETIMA, BUNGOMA

Kalameni mmoja kutoka hapa alitoroka boma lake akidai alikuwa akiwindwa na polo aliyeshuku kuwa mpango wa kando wa mke wake. 

Kulingana na mdokezi, polo alifunganya virago na kutorokea jijini huku akiwaacha wenyeji vinywa wazi.

Inadaiwa kalameni alimlaumu mkewe kwa masaibu yaliyomzonga.

“Mke wangu si mtu mzuri. Heri niondoke nimpe nafasi aendelee na raha yake. Sitaki kuuliwa hapa,” kalameni aliwaambia majirani.

Kipusa alijaribu kumzuia polo asiondoke lakini alilemewa nguvu na polo.

“Kazi yako ni mipango ya kando tu. Juzi umenitusi kuwa mimi sikutoshelezi ndio maana unakimbizana na vijana barobaro,” kalameni alimkaripia mkewe.

Kipusa alipinga madai ya polo huku akidai kuwa yalikuwa uongo mtupu.

“Wewe acha uongo wako. Huyo unayesema si mpenzi wangu bali ni jamaa yangu,” kipusa alijitetea.

Penyenye zinasema polo alikuwa akizozana na mkewe kuhusiana na tabia yake ya kuchovya nje.

Penyenye zilizotufikia zinasema polo alikuwa akipata jumbe za kumtishia maisha akiendelea kumgombeza mkewe.

“Juzi huyo jamaa alinisimamisha njiani na akanipa onyo kali. Aliniambia uhusiano wenu ulianza mkiwa shule ya msingi na nikiwa kizingiti nitanyoroshwa,” kalameni alimfokea mkewe.

Majirani walibaki kutazama sinema ya bure jamaa akifichua masaibu yake.

“Jana usiku nimesikia jamaa akitembea hapa nje. Najua ni mimi wanatafuta. Heri nikuachie boma uendelee na tabia zako nao,” polo alimueleza mkewe.

Baada ya kumaliza kupakia mizigo yake, polo aliitisha bodaboda na kuondoka akiapa kutorudi.

“Sitaki kupigwa na hao watu wako. Ukitaka kuwaleta hapa, basi una uhuru sasa,” polo alimueleza mkewe huku akienda.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Pendekezo rais ahudumu kwa miaka 4 na seneta miaka 7

Airtel yalemewa na biashara Afrika, yapanga kung’atuka

adminleo