• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 11:34 AM
Ukosefu wa maji Eastleigh wapandisha bei hadi Sh50 kwa mtungi

Ukosefu wa maji Eastleigh wapandisha bei hadi Sh50 kwa mtungi

Na PETER CHANGTOEK

UKOSEFU wa katika mitaa mingi jijini Nairobi, umekuwa ukiwatatiza mno wakazi wa mitaa husika. Watu wengi wamekuwa wakitatizika sana katika mitaa kama vile Eastleigh, Pangani, Ngara, South B, South C na Nairobi West.

Wengi hulazimika kuyanunua maji kutoka kwa wauzaji wanaobeba kwa mikokoteni, licha ya kuwa baadhi ya wauzaji hao huwa hawazingatii usafi unaofaa.

Hata hivyo, wengi wa wauzaji wa maji hayo huvuna pakubwa kutokana na changamoto hiyo ya ukosefu wa bidhaa hiyo, ambayo ni muhimu kwa uhai wa wanadamu.

Kwa mujibu wa baadhi ya wauzaji wa maji wanaoitumia mikokoteni kuyasambaza maji kwa wakazi wa mitaa kadha wa kadha jijini Nairobi, bei ya maji huwa juu katika mitaa mingineyo, kama vile Eastleigh.

“Sisi huuza kwa bei ya Sh50 kwa mtungi mmoja wa lita ishirini,” akadokeza mwuzaji mmoja, ambaye huyauza maji katika mtaa wa Eastleigh, kwa kuutumia mkokoteni.

Wengi wao huyanunua maji kutoka mtaani Majengo, Pumwani, kwa jumla ya Sh40-Sh70 kwa mkokoteni mmoja ulio na mitungi 30 hadi 70. Hii yamaanisha kuwa wao huuziwa maji mtungi mmoja wa lita 20 kwa Sh1, na wao hupata faida ya Sh49, kwa mtungi mmoja, wauzapo kwa Sh50, na endapo watayauza kwa Sh40, hupata faida ya Sh39 kwa mtungi mmoja.

Kwa jumla, wauzaji hao wa maji hupata faida ya Sh1,950-Sh2,450 kwa mkokoteni mmoja wenye maji mitungi ishirini.

Wakazi wengi waliozungumza na Taifa Leo Dijitali, waliomba serikali kusaidia kulitatua tatizo la maji ambalo limekuwa likiwakumba kwa muda mrefu sana.

You can share this post!

Mradi wa filamu watazamiwa kuiletea Fort Jesus Sh20 bilioni

Ageukia kilimo cha penino baada ya matundadamu kumpiga...