• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:03 AM
Majopo 15 yaliyoundwa na Rais yavunjwa na mahakama

Majopo 15 yaliyoundwa na Rais yavunjwa na mahakama

Na RICHARD MUNGUTI

MAJOPO 15 ambayo wanachama wake waliteuliwa na Rais Uhuru Kenyatta na mawaziri mbalimbali yatafutiliwa mbali kufuatia uamuzi wa Mahakama Kuu kwamba yanapasa kuteuliwa na Tume ya Kuajiri Watumishi wa Idara ya Mahakama (JSC).

Kufuatia uamuzi wa Jaji Maureen Onyango , majopo hayo yanapasa kuvunjwa kwa vile walioyateua hawana mamlaka kisheria.

Uamuzi huo wa Oktoba 30, 2020, ulioharamisha uteuzi wa wanachama watano wa jopo la kuamua mizozo ya wapangaji na wenye mijengo (BPRT) sasa umepingwa katika Mahakama ya rufaa na wakili Charles Kanjama akisema “ umesababisha hali ya taharuki na kizugumkuti.”

Huku akiomba mahakama hii ya pili kwa ukuu nchini ifafanue sheria inayomwezesha Rais na Mawaziri kuteua wanachama waa majopo ya kuamua mizozo katika idara za serikali, Bw Kanjama amesema suala hilo ni la dharura na halipasi kuchukuliwa kwa uzembe.

Bw Kanjama anayewakilisha wanachama wa BPRT anaomba mahakama ta rufaa isitishe kutekelezwa kwa agizo kwamba JSC iteue wanachama wa majopo kwa vile.

Wakili Kanjama ameeleza mahakama ya rufaa kuwa Waziri Jane Maina aliyeteua jopo la BPRT alikuwa anatekeleza jukumu lake kisheria sawia na Rais Kenyatta na mawaziri wengine walioteua majopo mengine 14.

Baadhi ya majopo yatakayoathiriwa ni lile linalothibiti mashirika ya serikali (State Corporations Appeals Tribunal), Jopo la masula ya ushuru, BPRT na mengine.

Bw Kanjama anaomba mahakama ua rufaa iwarejeshe kazini wanachama watano wa BPRT walioanza kazi Juni 2020.

Kufikia sasa jopo hilo la BPRT imesikiza kesi za ya 10,000.

Bw Kanjama amesea wapangaji na wenye nyumba za kibiashara na za kuishi wataendelea kuteseka hadi pale uamuzi kamili utakapotolewa kuhusu uhalali wa teuzi hizi za majopo.

Kesi ya kupinga uteuzi wa BPRT iliwasilishwa mahakanani na mawqakili Okello Odero na Ian Mwiti…

Katika mlalamishi yao mawakili hao walisema sheria ya thuluthi moja haikufuatwa na Waziri Betty Maina kwa vile alimteua mwanamke mmoja badala ya wawili na wanaume watatu.

Mahakkama ya rufaa itatoa uamuzi baada ya siku tatu.

You can share this post!

Polisi akana kumlaghai mfanyabiashara Sh3.9 milioni

Uchunguzi wa kifo cha Tecra Muigai kufanyika Februari