• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
LISHE: Mayai, bekoni na pancake

LISHE: Mayai, bekoni na pancake

Na MARGARET MAINA

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa kupika: Dakika 40

Walaji: 3

Vinavyohitajika

• mayai 5

• kijiko 1 cha siagi

• chumvi

• vikombe 2 unga wa ngano

• ¼ kikombe sukari

• vijiko 4 vya baking powder

• ½ kijiko cha chumvi

• vikombe 1? maziwa

• ¼ kikombe cha siagi iliyoyeyushwa

• vijiko 2 vya vanilla

• yai 1

• bekoni gramu 500

• mafuta ya kupikia

Maelekezo

Piga mayai, maziwa na chumvi kwenye bakuli, mpaka upate mchanganyiko.

Yeyusha siagi kwenye kikaangio kisichoshika chini katika moto wa chini. Ongeza mchanganyiko wa mayai. Chemsha kwa sekunde 20 bila kugeuza, kisha anza kukoroga. Koroga mpaka mayai yaive. Pakua.

Kwenye bakuli, chekecha unga wa ngano, sukari, baking powder na chumvi. Changanya.

Ongeza maziwa, siagi iliyoyeyushwa, vanilla na yai. Changanya vizuri mpaka ulainike vizuri.

Kwenye kikaangio kisichoshika chini, katika moto wa chini, paka kikaangio siagi.

Mwaga unga wa robo kikombe kwenye kikaangio. Pika mpaka upande wa chini uwe kahawia; geuza na upike upande mwingine. Pakua.

Ondoa bekoni kwenye karatasi.

Kwenye kikaangio kisichoshika chini, weka mafuta ya kupikia yachemke kwenye moto wa juu.

Ziweke bekoni moja baada ya nyingine kwenye mafuta na upike huku ukizigeuza kwa dakika nane.

Pakua na ufurahie.

You can share this post!

MKU yapata wahitimu wengi wa somo la sheria – ripoti

Ripoti ya ‘Production Gap’ yapendekeza mataifa...