• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Sonko amnunulia mwanawe wa miaka 6 Mercedes Benz kwa bathidei

Sonko amnunulia mwanawe wa miaka 6 Mercedes Benz kwa bathidei

Na CHRIS ADUNGO

LICHA ya habari kuenea kuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko anaendesha shughuli za kaunti kutoka kaunti ya Machakos, hilo halijamzuia kuendelea na maisha yake ya kawaida.

Hii ni baada ya kumwaga mamilioni sokoni kumnunulia mwanawe wa kupanga,  Satrine Osinya, zawadi ya kipekee siku yake ya kuzaliwa.

Sonko alidhihirisha mapenzi kwa mwanawe huyo kwa kumnunulia shangingi aina ya Mercedes Benz Sport ambalo litatumika kumzungusha jijini Nairobi kufurahia siku hiyo muhimu kwa maisha yake.

Picha zilizowekwa kwa mitandao ya kijamii na mkewe gavana huyo, Primrose Mbuvi zinaonyesha mvulana huyo wa miaka sita akipambwa kwa kila aina ya zawadi kwenye sherehe ya bathidei.

“Kijana wa bathidei alifurahi sana, tunakusherehekea mwanangu, Mola ni mwaminifu,” akaandika Bi Mbuvi.

Karamu hiyo inaaminika kuhudhuriwa na watuwa familia na marafiki wa karibu wa mtoto huyo pekee.

Gavana Sonko aliamua kumlea Satrine baada ya mamaye kufariki katika kanisa la Likoni kufuatia shambulizi la kigaidi mnamo Machi 23, 2014.

Sonko pia alijitwika jukumu la kumlea kakaye mkubwa Satrine, Moses Gift Osinya, ambaye ajiunga na shule ya upili ya kitaifa ya Lenana, Nairobi hapo 2017.

 

You can share this post!

Sielewi nilikuwa nafikiria nini nikianguka kwa eskaleta...

Ushuru yaikaribia Stima kileleni mwa jedwali Supa Ligi

adminleo