• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:45 AM
Serikali ndiyo chanzo cha migomo shuleni – KUPPET

Serikali ndiyo chanzo cha migomo shuleni – KUPPET

Na Gaitano Pessa

KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu wa Vyuo Anuwai (KUPPET) ameilaumu serikali kwa kuwa kiini kikuu cha kuongezeka kwa mioto shuleni.

Bw Misori (pichani) alisema kwamba wimbi la uchomaji shule lililopo limechangiwa na hali sawa, ila serikali imeshindwa kuidhibiti.

Akizungumza Jumamosi mjini Busia kwenye mkutano wa kila mwaka wa chama, Bw Misori alisema kuwa sababu kuu za mioto hiyo ni matatizo ya masuala ya usimamizi ambayo serikali imeshindwa kuyatatua. Vile vile, alitaja hali mbaya ya miundomsingi kama kiini kingine kikuu.

“Hatuhitaji uchunguzi kufahamu kiini kikuu cha hali ya mioto na migomo shuleni. Serikali imechangia moja kwa moja, kwani mazingira ya masomo katika shule husika yako katika hali mbaya sana,” akasema.

Akaongeza: “Ni vipi utawaeleza wanafunzi kuendelea kukaa katika shule ya mabweni ambayo haina vyumba vya malazi, kumbi za maakuli na madarasa ya kutosha. Serikali inapaswa kuchukua lawama moja kwa moja.”

Katibu huyo alikuwa ameandamana na Mwakilishi wa Wanawaka katika kaunti hiyo, Catherine Wambilianga, msimamizi mkuu wa tawi hilo Mophat Okisai na maafisa kutoka kaunti jirani.

Bi Wambilianga, aliye pia ni Katibu wa Mipango katika chama alisema kuwa imefikia wakati ambapo lazima serikali imalize kimya chake kuhusu mioto hiyo.

“Tunakabiliwa na changamoto hizi kwa kuwa serikali imekataa kutoa Sh5 kwa shule, ili zitumiwe katika uimarishaji wa miundosmsingi husika. Hilo ndilo limezua hali ya kutotosheka miongoni mwa wanafunzi. Serikali inaonekana kusahau kwamba si walimu wanachangia wala kuwachochea wanafunzi,” akaongeza.

Aliapa kuhakikisha kwamba changamoto zote zinazowakabili walimu zimejadiliwa katika Bunge la Kitaifa.

You can share this post!

Miili ya wafu isiyo na wenyewe yatatiza hospitali ya Thika...

Familia ya polisi ‘aliyejiua’ yadai haki

adminleo