• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:25 PM
Chelsea sasa yataka usogora wa Ramsey

Chelsea sasa yataka usogora wa Ramsey

Na AFP

CHELSEA iko tayari kuipiku Liverpool katika juhudi za kupata huduma za mchezaji wa Arsenal, Aaron Ramsey kabla ya soko kufungwa Agosti 9 kwa kutoa Sh4.5 bilioni.


Kiungo huyu kutoka Wales yuko katika mwaka wa mwisho kwenye kandarasi yake na Arsenal iko tayari kupata fedha za kujiimarisha kwa kumuuza.


Gumzo linadai kwamba kocha wa Chelsea, Maurizio Sarri amekubali hawezi kupata sahihi ya mchezaji wa Aston Villa, Jack Grealish, ambaye ataelekea Tottenham, ikifanikiwa kumshawishi, ili ashiriki Klabu Bingwa Ulaya.


Sarri, ambaye hakuweza kunyakua wachezaji kadhaa aliotaka kutoka Italia, atamgeukia Ramsey, ambaye hajaongeza kandarasi yake ugani Emirates.

You can share this post!

Nusra afutwe kazi kwa kuonja mlo wa mdosi

Barcelona, PSG na Juventus kivumbini kumsajili Pogba

adminleo