• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Msiidharau Tunisia, meneja wa Simbas aonya

Msiidharau Tunisia, meneja wa Simbas aonya

Na GEOFFREY ANENE

SAA chache baada ya Tunisia kutua jijini Nairobi, Meneja wa timu ya Kenya ya raga ya wachezaji 15 kila upande ya wanaume ameonya vijana wake dhidi ya kudharau Waarabu hao watakapokutana uwanjani RFUEA hapo Agosti 11, 2018.

Katika mahojiano ya simu jijini Nairobi mnamo Agosti 6, Wangila Simiyu amesema Kenya Simbas haifai kuchukulia mechi hiyo yake ya nne ya Kombe la Afrika kuwa “mswaki.”

“Licha ya kupondwa na Namibia (118-0) na Uganda (67-12), Tunisia haifai kudharauliwa hata kidogo. Ilibabaisha Zimbabwe na hata kuwachapa (18-14). Itakumbukwa kwamba Zimbabwe ilitusumbua sana ilipozuru Nairobi. Tunastahili kuheshimu Tunisia na kuchukulia mechi hiyo kwa uzito unaofaa,” Wangila amesema.

Kenya itaanza mchuano huu na asilimia kubwa ya kuushinda. Ina rekodi nzuri katika ardhi yake dhidi ya Tunisia. Julai 8 mwaka 2017 katika kombe hili jijini Nairobi.

Simbas imerarua Tunisia mara sita jijini Nairobi. Iliwika 100-10 Julai 8 mwaka 2017. Kabla ya hapo, ilikuwa imecharaza Waarabu hawa 46-15 mwaka 2015, ikawalima 31-24 mwaka 2012, ikawachapa 16-7 mwaka 2011, ikawakanyaga 25-21 Juni 10 mwaka 2006 na kuwalaza 37-15 Mei 21 mwaka 2005.

Ushindi mbili ambazo Tunisia imepata dhidi ya Kenya tangu mwaka 2000 zimekuwa nchini Tunisia. Ilizaba Kenya 44-15 Agosti 2 mwaka 2008 jijini Tunis na kuilima tena 31-12 Septemba 16 mwaka 2006 jijini humo.

Katika kipute cha mwaka 2018, ambacho pia kinatumika kama mchujo wa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2019, Namibia inaongoza kwa alama 20.

Kenya ni ya pili kwa alama 12. Uganda, Tunisia na Zimbabwe zinafuatana katika nafasi za tatu, nne na tano kwa alama tano, nne na tatu, mtawalia. Morocco inavuta mkia kwa alama tatu.

Inatofautiana na Zimbabwe kwa ubora wa magoli. Namibia na Zimbabwe zimesakata mechi nne kila mmoja. Kenya, Uganda, Tunisia na Morocco zimecheza mechi tatu kila mmoja.

Matokeo na ratiba:

Juni 16

Namibia 55-6 Uganda

Zimbabwe 23-23 Morocco

Juni 23

Namibia 118-0 Tunisia

Morocco 24-28 Kenya

Juni 30

Kenya 45-36 Zimbabwe

Morocco 7-63 Namibia

Julai 7

Kenya 38-22 Uganda

Tunisia 18-14 Zimbabwe

Agosti 4

Uganda 67-12 Tunisia

Zimbabwe 28-58 Namibia

Agosti 11

Uganda na Morocco

Kenya na Tunisia

Agosti 18

Tunisia na Morocco

Namibia na Kenya

Uganda na Zimbabwe.

You can share this post!

Kabonyo yatia mfukoni Sh300,000 kwa kushinda Opich Pacho

Timu ya handiboli yaelekea Rwanda kusaka ubingwa wa Afrika

adminleo