• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Gor kunufaika na Sh12m kwa mauzo ya Walusimbi

Gor kunufaika na Sh12m kwa mauzo ya Walusimbi

NA CECIL ODONGO

MABINGWA mara 16 wa ligi ya KPL Gor Mahia, watavuna Sh12 milioni kutokanana na mauzo wa aliyekuwa mlinzi wao raia wa Uganda Godfrey Walusimbi kwa mibabe wa soka ya Afrika Kusin, Kaizer Chiefs.

Gor walisalimu amri katika juhudi zao za kumtaka Walusimbi  asalie klabuni na sasa watapokezwa kitita hicho kikubwa na washiriki hao wa ligi ya Absa baada ya pande zote mbili kuhitimisha makubaliano kuhusu uhamisho wa sogora huyo.

“Hakuna utata wowote kati yetu na Gor Mahia tena kuhusiana na hatua yetu ya kusaini beki wa Godfrey Walusimbi. Tumekuwa na majadiliano mapana yaliyohusisha wahusika wote na kuafikiana kuhusu dili tutakayowatangazia hivi kabla ya mwisho wa mwezi Agosti,” akasema Afisa Mkuu Mtendaji wa Kaizer Chiefs Bobby Motaung.

Walusimbi sasa atawagaragazia Chiefs baada ya kupokezwa cheti kinachoidhinisha uhamisho wake kabla ya mwisho wa mwezi wa Agosti huku fedha za uhamisho wake zikikabidhiwa mabingwa hao watetezi wa KPL  katika kipindi hicho.

You can share this post!

Wabunge wafika kortini kumliwaza mwenzao aliyeshtakiwa kwa...

Wasanii 21,000 wavuna Sh200m kwa Safaricom

adminleo