• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
Wasanii 21,000 wavuna Sh200m kwa Safaricom

Wasanii 21,000 wavuna Sh200m kwa Safaricom

Na BERNARDINE MUTANU

Wanamuziki na wasanii wamefaidika kutokana na Sh200 milioni kutokana na Safaricom baada ya mauzo ya nyimbo zao kupitia kwa mpango wa Skiza.

Mkuu wa uhusiano mwema Safaricom Steve Chege alisema wasanii kufikia 21,000 waliojisajili Skiza Tunes wananufaika na mauzo hayo.

Kampuni hiyo imekuwa ikitengeneza kiwango hicho cha fedha kila mwezi, alisema Bw Chege.

Aliongeza kuwa jukwaa hilo limewasaidia wasanii kupata pesa kutokana na mapato yao kwa kuuza nyimbo kwa wateja wa kupiga simu.

Kulingana na afisa huyo, Safaricom itazidi kuhamasiha wanamuziki nchini, “Safaricom imejitolea kuwekeza zaidi katika sekta ya muziki. Tulichukua hatua kuwawezesha wasanii kujipa pato,” alisema.

Safaricom mwaka jana ilitangaza ongezeko la asilimia 36 ya mapato kwa wasanii kutokana na mauzo ya muziki wao kwenye jukwaa la SKIZA.

You can share this post!

Gor kunufaika na Sh12m kwa mauzo ya Walusimbi

UFISADI: Rais wa zamani wa Korea Kusini kuozea jela

adminleo