• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 7:53 PM
Ajuta kujaribu kumtia mumewe kiganjani

Ajuta kujaribu kumtia mumewe kiganjani

Na LEAH MAKENA

GITEMBENE, MERU

Mama wa hapa alipatiwa talaka  kwa kuweka akiba kisiri ili ajenge nyumba ya kifahari. Mama alikuwa na mshahara mnono na akaamua kuweka pesa akiwa na lengo la  kujenga nyumba na kumweleza mumewe baada ya kuikamilisha. 

Mumewe hakuwa na kazi nzuri na mapato yake yalikuwa kidogo mno.

“Nia ya mama ilikuwa kumpunguzia mumewe mzigo kwa sababu mapato yake yalikuwa ya chini sana. Alitaka familia yake kuwa na maisha mazuri,” alisema mdokezi.

Inasemekana kuwa mama alichukua mkopo  benki ili kuharakisha ujenzi wa nyumba hiyo na akaamua kulipa madeni yote bila kumhusisha polo.

Haikujulikana jinsi mumewe alivyogundua siri ya mama ila alimpigia simu akiwa kazini na kumtaka kujipanga kuondoka kwake.

Jioni ya kisanga, mama alifika na kupata begi la nguo nje huku jamaa akitetemeka kwa hasira.

“Yaani unanifanya kutoa jasho kushughulikia mahitaji yote ya nyumbani ilhali unachukua loni kujengea uwapendao majumba makubwa? Huu uwe mwisho wangu na wewe kwani umekuwa kero kwangu,” jamaa aliteta.

Juhudi za mama za kujaribu kujitetea hazikufua dafu kwani polo aliendelea kubishana akidai jengo lililokuwa likikamilika halikuwa lao.

“Siwezi kuishi katika nyumba ambayo sikuhusika kujenga. Ulikuwa unaficha nini iwapo ulikuwa na nia nzuri?” mzee aliwaka.

Ilibidi mama kuzoa kilichokuwa chake na kuondoka huku polo akiapa kulisha watoto pekee yake na kumlaumu mkewe kwa kuficha siri kubwa kama hiyo.

Haikujulikana iwapo jamaa alibadilisha nia  baadaye mkewe kuwajulisha wazee wazungumze naye apate kujua ukweli wa mambo.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Ninavuta bangi ili nipate nguvu za kuchapa kazi shambani,...

Kikao cha Ruto na Kibwana chazua msisimko

adminleo