Pasta ‘azirai’ kuhepa kahaba aliyefika kudai hela za uroda
PASTA mmoja mtaani hapa alijifanya amezimia kuepuka aibu kahaba aliyemhudumia kwa mkopo kwenye danguro moja mjini alipomfuata kwake kudai haki yake.
Mhubiri huyo kamwe hakuamini kahaba huyo angemfuata hadi nyumbani anakoishi na familia yake kudai malipo kwa huduma ya aibu.
Ni kutokana na ufahamu kwamba aibu yake imefichuka kwani mkewe pia alikuwa karibu na mlango aliosimama kahaba huyo ambapo alijiangusha na kujifanya kuzimia.
“Mimi sikuwa na lengo la kuja kumpa presha. Nimekuja tu kudai malipo. Ni haki yangu. Nilimkopesha huduma huyu,” alifunguka kahaba huyo na kuondoka kisha jamaa akajiinua.
Haijulikani endapo baadaye alilipa deni hilo au kahaba alimhurumia na kumsamehe.