Habari za Kitaifa

Gavana Kawira aona mwangaza baada ya korti kusimamisha kubanduliwa kwake

Na HARRY MISIKO August 21st, 2024 1 min read

KAWIRA Mwangaza, ambaye alitumbukia kwenye giza Jumanne usiku, Agosto 20, 2024 baada ya kupoteza kiti chake cha ugavana, ameona miale ya mwangaza baada ya kwenda kortini.

Mahakama Kuu Jumatano asubuhi, Agosti 21, 2024 ilisimamisha uamuzi wa Seneti wa kumuondoa afisini kufuatia kutimuliwa na bunge la kaunti.

Jaji Bahati Mwamuye, ambaye aliidhinisha ombi la Bi Mwangaza kuwa la dharura, alisema kesi yake iliibua masuala mazito ambayo yanapaswa kusikilizwa na kuamuliwa na mahakama.

“Baada ya kuzingatia hayo, nimeridhika kwamba ombi hilo linaibua masuala ya kikatiba, kisheria na ya kweli ambayo yanahitaji mahakama hii kuingilia kati mara moja kwa kutoa agizo la muda la kusimamisha uamuzi wa seneti,” aliamua.

Habari zaidi kufuata