• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 PM
Dereva aliyemsaidia mama kujifungua atuzwa

Dereva aliyemsaidia mama kujifungua atuzwa

Na CHRIS ADUNGO

DEREVA aliyemsaida abiria mama mjamzito kujifungua katika barabara kuu ya Thika ametuzwa likizo yabei ghali na kampuni moja ya utalii humu nchini.

Mwanamke huyo, Philomena Mbithi, alisimulia jinsi dereva huyo, George Kariuki, alimsaidia kujifungua mtoto wa kiume baada ya kupatwa na uchungu wa uchu wa kujifungua baada ya kuabiri basi linalomilikiwa na kampuni ya 44 Company Sacco.

Dereva huyo, ambaye alikuwa anakumbushwa na kondakta kuhusu alivyokuwa akiendelea mama huyo ndani ya basi, alisitisha shughuli zote na kumsaidia mama huyo akajifungua.

 

Dereva huyo na kondakta wake wamemiminiwa sifa na Wakenya mitandaoni kwa ujasiri wao ambao ulitambuliwa na kampuni ya utalii ya Bonfire Adventures.

Ijumaa, kampuni hiyo iliamua kumtunuku dereva huyo likizo iliyolipiwa kupitia akaunti yake ya Twitter.

“Shujaa wa kweli – dereva aliyesaidia mama kujifungua mtoto salama. Hiki ni kitendo cha ukarimu na wakati tunasherehekea mashujaa wetu, tungependa kumpongeza dereva huyo kwa kumpa likizo. Tupe maoni ni wapi pazuri zaidi anafaa kuzuru,” ikasema taarifa ya kampuni hiyo.

 

You can share this post!

Ssimbwa ajiuzulu akilalamikia wachezaji kumgomea

Shujaa yalemewa na Fiji kwenye fainali

adminleo