• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 3:31 PM
Kaunti yawapa chakula ombaomba kama njia ya kuwataka wasijazane mjini

Kaunti yawapa chakula ombaomba kama njia ya kuwataka wasijazane mjini

Na WINNIE ATIENO

WAKATI huu wa janga la Covid-19 ni kipindi ambacho familia za kurandaranda na wale wa kuombaomba wanaendelea kumiminika Kaunti ya Mombasa kuomba chakula na pesa.

Hii ni kufuatia makali ya maisha yaliyoletwa na athari za virusi vya corona.

Kulingana na serikali zaidi ya watu laki 300,000 nchini wamepoteza ajira kufuatia athari za janga la corona huku biashara nyingi na hata hoteli zikifungwa.

Hata hivyo, serikali ya Kaunti ya Mombasa imeweka mikakati kuwaokoa wakazi hao kwa kuwapa vyakula ili warudi makwao.

“Tumebaini familia nyingi zinamiminika katikati mwa jiji la Mombasa kuomba vyakula na pesa kufuatia janga la corona ambalo limesababisha wengi kupoteza ajira,” alisema Bw Innocent Mugabe afisa wa kaunti anayesimamia lishe.

Kulingana na takwimu za kaunti, kuna takriban familia 1,809 za kurandaranda jiji hilo la kitalii.

Serikali ya kaunti hiyo ilishindwa kudhibiti na kukabiliana na idadi kubwa ya familia za kurandaranda na wale ombaomba hususan wakati huu wa janga la ugonjwa wa Covid-19.

Hata hivyo wadadisi wameonya kwamba wamo katika hatari ya maambukizi ya virusi vya corona wakisalia bila makao.

“Tunataka watu wa familia waache kujazana katikati mwa jiji kutokana kwa sababu wanajiweka katika hatari ya virusi vya corona. Tunawapa vyakula ili wasalie majumbani mwao ambako wako salama zaidi,” aliongeza Bw Mugabe.

Familia 200 za kurandaranda zinaendelea kunufaika na shughuli hiyo.

You can share this post!

Biashara zajiandaa kufungua

WASONGA: Mabadiliko ya katiba hayatamaliza ghasia

adminleo