• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 5:45 AM
Ruto aingiwa na baridi kesi yake ya ICC ikifufuliwa

Ruto aingiwa na baridi kesi yake ya ICC ikifufuliwa

Na BENSON MATHEKA

?HATUA ya Naibu Rais William Ruto ya kusitisha mikutano yake ya kisiasa, imeibua hofu kwamba, ameingiza baridi kufuatia matukio ya hivi majuzi ikiwa ni pamoja na hofu ya kufufuliwa kwa kesi iliyomkabili katika Mahakama ya Kimataifa kuhusu Uhalifu (ICC).?

Mnamo Jumanne wiki jana, Dkt Ruto alitangaza kuwa amefuta mikutano ya kampeni yake ya kusaidia walala hoi kufuatia ongezeko la maambukizi ya virusi vya corona nchini.

“Kuongezeka kwa maambukizi ya corona kuna hatari ya kuzuka kwa mkumbo wa pili wa msambao wa virusi hivyo. Kwa sababu hii, nimeamua kusitisha hafla zangu za umma hadi nitakapotangaza,” Dkt Ruto alisema.

Tangazo hilo lilijiri siku moja baada ya ICC kutangaza kuwa wakili Paul Gicheru aliyekuwa akisakwa kwa miaka mitano kwa madai ya kuhonga mashahidi wa kesi ya ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007 dhidi ya Ruto kujisalimisha.

Ingawa Dkt Ruto alisema aliahirisha mikutano yake aliyopanga Makueni, Machakos na Kitui kufuatia ongezeko la maambukizi ya corona, maswali yameibuka kuhusu sadfa ya hatua hiyo na kujisalimisha kwa Bw Gicheru huko ICC.

Kuna wasiwasi kwamba, kujisalimisha kwa wakili huyo ICC ambako hakukutarajiwa, kunaweza kuvuruga azima ya Dkt Ruto ya kugombea urais 2022.

You can share this post!

Kamala Harris aalika wanawake zaidi kuwania viti vya kisiasa

Magoha kuandaa kikao kujadili ratiba mpya ya shule